Kutakuwa Mwanga
Kutakuwa mwanga nyumbani mwa Bwana,
Nifikapo mwisho wa mwendo;
Nitapata raha mkononi mwa Bwana,
Nifikapo mwisho wa mwendo.
Safari ikomapo siku ya mwisho,
Nitakaribishwa na pendo;
Kwa kuwa Mwokozi ananingojea,
Nifikapo mwisho wa mwendo.
Sitazikumbuka taabu za njiani,
Nifikapo mwisho wa mwendo;
Sitawakumbuka walionipinga,
Nifikapo mwisho wa mwendo.
Nimwone rafiki aliye Mwokozi,
Nifikipo mwisho wa mwendo;
Hivyo natamani katika mbinguni,
Nifikapo mwisho wa mwendo.
Lyrics Submitted by Wapang'ana Abraham
Lyrics provided by https://damnlyrics.com/