Nitawapumzisha

Mary Atieno

Njooni kwangu nyinyi nyote ,msumbukao na mizigo mizito
msifadhaike nitawapumzisha,Nira yangu ni laaini
mzigo wangu ni mwepesi mno
jifundusheni kwangu mimi ni mpole .

Njooni mlio vunjika mioyo
njooni wenye mioyo mizito
nitawaganga niwaponya
nitawapa furaha,
mimi ni baba wa yatima ,
njooni nyote mnaolia,
niwajaza na roho wangu nitawafariji

Msiogope kwa sababu ,nyinyi ni bora kuliko kondoo
mmewashinda mashomoro sitawasahau
Nimesikia kilio chenu nitayavuta machozi yenu yote
nitawashika mikono nitawasaidia

Tafuteni ufalme wangu, utafuteni uso wangu
nitawajaza kila mnacho hitaji
njooni kwangu maskini nitawapa utajiri wangu
njooni wenye dhambi nitawaokoa

Lyrics Submitted by kenneth Micheni Duncan

Lyrics provided by https://damnlyrics.com/