damnlyrics.com

Chozi La Damu

Watoto wa nyumba zote njooni tuungane

Tuwalilie wazazi chozi la damu

Tupaaze sauti zetu za majonzi na kwikwi

Kwa wachache wenye huruma watatusikia

Haki ya malezi bora tumenyang'anywa

Urithi wa maadili tumefutiwa

Oh dunia dunia, dunia unatutesa

Oh dunia dunia, tumekukosea nini

Oh dunia dunia, mbona hupendi watoto

Oh dunia dunia, sikia kilio chetu

1. Oh dada zetu na mama zetu, tunajua mnajipenda

Ingawaje tungetamani na sisi mtufikirie

Mavazi mnayovaa leo yanatufundisha nini

Mnafikiria nini kwa kizazi mnachokilea

Msije mkashangaa dunia siku zinazokuja

Viwanda vyote vya nguo vitakapofungwa

2. Oh kila siku tunapolala baba zetu hamjarudi

Asubuhi tukiamka, baba zetu mmeondoka

Siku tukibahatika kushtuka usiku wa giza

Tunachokishuhudia ni mama anapigwa makofi

Na vitisho vya talaka matusi na harufu ya pombe

Darasa gani mnatupa watoto wenu

3. Oh tukirudi toka shuleni, madaftari hamkagui

Eti kwa kuwa tumechoka, burudani mwatuwekea

Video mnazowasha picha za vita na mauaji

Au mikanda iliyorekodiwa Sodom na Gomora

Hamkumbuki ya kuwa mnayafuta ya darasani

Urithi gani mnatupa wazazi wetu

4. Oh kwenye chakula cha usiku, siku zote baba hayuko,

Kusali sala za pamoja, kwenye nyumba yetu ni mwiko,

Amechelewa kutoka kwa mama mdogo yule wa siri

Au giza likizidi, hatarudi mpaka asubuhi

Na mama akishajua mbio kwa Anko wa usiseme`

Familia moja baba na mama watano

5. Oh kwa sababu ya mambo haya, ndugu zetu wanaumia

Wapo wanaorandaranda mitaani bila makazi

Wengi wamelazimika kuajiriwa bado wadogo

Hawana tena nafasi ya kusoma wapate elimu

Na wengi wanajiuza miili yao ili waishi

Mbona dunia umetugeuka watoto

Enjoy the lyrics !!!