damnlyrics.com

Mlango Uko Wa Wema

[1] Mlango uko wa wema, Mlango wazi huo

Yesu ameufungua, na hakuna kufungwa!

Mlango wazi, ajabu, uliachwa wazi kwangu!

Kwangu, Kwangu, Kwangu!.... Wazi, wazi kwangu!

[2] Mlango hukaa wazi watu waokolewe:

Masikini na matajiri, wa mataifa yote!

[3] Maajabu mlango wazi, Rafiki kaza mwendo;

Msalaba ukubali, amana ya upendo!

[4] Msalaba tutabeba, daima na furaha!

‘pendo la Yesu hushinda, Tunainama kwake!

Lyrics Submitted by Paul Munyao Musya

Enjoy the lyrics !!!