damnlyrics.com

Ndoa

Mlilelewa na wazazi, sasa mmekua

ndio maana mmeamua kuanza maisha yenu.

Mmeaacha baba na mama kuwa mwili mmoja

Ndoa yenu ni takatifu, Mtu asiwatenge

Bila shaka mmejifunza mambo mbali mbali

japokua mmepitia vipindi tofauti.

Katika yote hayo Mshukuruni Mungu x2

kwa kua amewafikisha hapa mlipo x2

Safari yenu ya ndoa, mmeianza kwa imani

ndio maana mwategemea matokeo mazuri.

Yale mtakayotatua mshukuruni Mungu na yatakayowashinda mlilieni pamoja

Imani yenu yote iwekeni kwa Mungu

msiweke katika vitu, shetani asije ona

Akipiga hivyo vitu imani yenu itayumba

Imani yenu ikiyumba nanyi mtayumba

Na ndoa yenu nayo itayumba x2

Neema ikawafunike

yeye Bwana akawe mwalimu wenu

Mungu wenu akawe mshauri wenu

Ndoa ni kama kama jua lenye mwangaza mwanana

Kila lichomozapo wengi hulifurahia

watu makundi makundi hulisifia sana

jua hili jua zuri lina faida kwa afya

Ila jua lilelile likifika mchana,

wengi hulalamika na kulikimbia

Joto likiwazidia wananung'unika x2

Wanasahau walilisifia asubuhi x2

Jua likifika jioni faraja hurejea tena

Ila bahati mbaya jua laenda kuzama

Hapo sifa za asubuhi huanza kusikika upya

walovumilia mchana hula matunda yake

Ila tunawaombea Mungu awatetee

Mtakapofika mchana mkavumiliane

Joto likiwazidia mkasameheane

Msilipize kisasi msije kujidhuru.

Mkakumbuke jioni ya amani yaja x 2

Kama kuna jema lolote msisite kulifanya.

Na neno la Msamaha msilicheleweshe

Mkaishi Maisha yenu, Msiige ya wengine

Epukeni mazoea yanaleta kiburi

Tena maneno mabaya uharibu tabia

kamwe msije thubutu kuyatunza moyoni.

Ndoa ni kipindi cha mwisho cha maisha ya watu

Kitumieni vizuri kwa kua ni kifupi

Maana hamjui lini kifo kitawatenga x2

Mtendee wema mwenzako kadiri utakavyoweza

Moyo unaweza kataa ila jilazimishe

Kama ukitenda wema huna utakachopoteza

Mtendee akiwa hai macho yake yanaona

wengi wanajilaumu kua walikosea

wakati wa kutenda wema wao waliumiza

Mungu akawatenganisha hawaishi pamoja

Wanatamani watende wema ila walichelewa

Maana wenzao hawapo tena x2

Mmeugusa moyo wa Mungu kwa kutimiza agano lake.

Lyrics Submitted by Mpeli M Mwakyeja

Enjoy the lyrics !!!