damnlyrics.com

Yesu Kwetu Ni Rafiki

YESU KWETU NI RAFIKI: Lyrics Posted by Andrew Kandie Kimuge-0726653432

1.Yesu kwetu ni rafiki, Huambiwa haja pia;

Tukiomba kwa Babaye Maombi asikia;

Lakini twajikosesha, Twajitweka vibaya;

Kwamba tulimwomba Mungu Dua angesikia.

2. Una dhiki na maonjo? Una mashaka pia.

Haifai kufa moyo, Dua atasikia

Hakuna mwingine mwema Wa kutuhurumia;

Atujua tu dhaifu; Maombi asikia.

3. Je, hunayo hata nguvu, Huwezi kuendelea,

Ujapodharauliwa Ujaporushwa pia,

Watu wange kudharau,

Wapendao dunia, Hukwambata mikononi, Dua atasikia.

Lyrics Submitted by Lyrics Posted by Andrew Kandie Kimuge-0726653432

Enjoy the lyrics !!!