DamnLyrics - The center provides all the lyrics

Mteule Uwe Macho - ROSE MUHANDO



     
Page format: Left Center Right
Direct link:
BB code:
Embed:

Mteule Uwe Macho Lyrics


Mteule Uwe Macho – Rose Muhando
1. Ooh ye dunia sasa imashakani
Kumbe dhambi imekuwa kitu cha kushangiliwa
Makala makubwa imejengewa ngome za kifahari
Ooh ye dunia sasa imashakani
Kumbe dhambi imekuwa kitu cha kushangiliwa
Makala makubwa imejengewa ngome za kifahari
Mabomu ya kujitoa muhanga ni jambo la hatari
Wakati damu hiyo hatia ni jambo la kutisha
Yaliyonenwa na nabii Danieli sasa yanatimia
Ni nani atasimama, mbele ya hasira ya Bwana
Atulize ghadhabu yake isiipate dunia
Ni nani atasimama, mbele ya hasira ya Bwana
Atulize ghadhabu yake isiipate dunia
Eeeh, lelelelelelele
Mteule uwe maaaacho
Ni siku za mwisho nasema
Chorus:

Mteule uwe macho, hizi ni siku za mwisho
Kwani yale yaliyotabiriwa sasa yanatimia
Tusimame imara tujifungeni miganda
kwa silaha za haki kifuani, na tusonge mbele
Mpigeni shetani, mnyang’anye mamlaka
Tupilia mbali tamaa ya dhambi, weka pembeni
Uwe macho, hizi ni siku za mwisho
Kwani yale yaliyotabiriwa sasa yanatimia
Tusimame imara tujifungeni miganda
kwa silaha za haki kifuani, na tusonge mbele
Mpingeni shetani, mnyang’anye mamlaka
Tupilia mbali tamaa ya dhambi, Weka pembeni
2. Kutangatanga kwako wewe, mbona kwa kuchelewesha
Nachelewa kusema nawe, utafuna ulichopanda
Shika sana ulicho nacho, Yesu yu karibu kucha
Mwenye sikio asikie, roho asema na kanisa
Eeeh, lelelelelelele
Ah yayayayaya
(Eh, mwenye dhambi wewe, endelea kutenda dhambi)
Muongo endelea kutenda dhambi, dunia ikujuee
(Eh, mwenye dhambi wewe, endelea kutenda dhambi)
Mumbea endelea kusema umbea, vunja nyumba za watu
(Eh, mwenye dhambi wewe, endelea kutenda dhambi)
Mchawi endelea kuroga sana, mchana wewee
(Eh, mwenye dhambi wewe, endelea kutenda dhambi)
3. Wachungaji tuelezeni, mwatupeleka wapi jamani
Mbona bishopu mwanamume, ameoa mume mwenzie
Andiko hili latoka wapi, tena kwenye Bibilia gani
Watoto wetu wa kiume, tuwafiche wapi jamani
Wamama nao bila aibu, wazini na vijana wadogo
Sasa tutapataje kupona, ukimwi utatumaliza
Eeeh, lelelelelelele
Ah yayayayaya
(Eh, mwenye dhambi wewe, endelea kutenda dhambi)
Kahaba endelea kufanya ukahaba, mpaka kwenye internet
(Eh, mwenye dhambi wewe, endelea kutenda dhambi)
Malaya endelea kufanya umalaya, utakwenda na bomu
(Eh, mwenye dhambi wewe, endelea kutenda dhambi)
Washerati endelea kufanya dhambi, Yesu yuaja
(Eh, mwenye dhambi wewe, endelea kutenda dhambi)
Lokole endelea kujitakaza, Yesu yuaja
(Eh, mwenye dhambi wewe, endelea kutenda dhambi)
Shoga endelea kufanya ushoga, mpaka kwenye mtandao
(Eh, mwenye dhambi wewe, endelea kutenda dhambi)
Eeeh, lelelelele
Jamani nasema
Chorus:
Mteule uwe macho, hizi ni siku za mwisho
Kwani yale yaliyotabiriwa sasa, yanatimia
Tusimame imara, tujifungeni miganda
kwa silaha za haki kifuani, na tusonge mbele
Mpigeni shetani, mnyang’anye mamlaka
Tupilia mbali tamaa ya dhambi, weka pembeni
Uwe macho
Oh, yeyeye, yeyeye
Oh yeyeyeye
Uh yeyeyeyeye
Lyrics Submitted by Dennis Mulongo

Enjoy the lyrics !!!