Amebarikiwa - Pst Alex & Mary Atieno Ominde
| Page format: |
Amebarikiwa Lyrics
Amebarikiwa anyemtumaini Jehova Mungu Baba X2
Atakulisha atakunywesha kweli atakuvisha X2
Jamii yako yote itabarikiwa kamwe hutapungukiwa X2
Omba Jehova Mungu Wako kwa moyo wako wote atakupa ajaze moyo wako hatakuaibisha X2
Amebarikiwa anayetafuta uso wake Mungu Baba X2
Atakuonyesha mambo makubwa magumu usiyoyajua X2
Atakuponya atakufunulia ukweli na amani tele X2
Usichoke kutafuta uso wake Mungu Baba atakupa chochote utakacho yeye ni mwaminifu
Bwana anasikia maombi ya wenye haki atajibu Bwana hatawanyima kitu chochote
Amebarikiwa anayetafuta uso wake Mungu Baba X2
Atakufunika na mabawa yake Baba atakulinda X2
Atakuonyesha wokovu wake utaishi siku nyingi X2
Usichoke kutafuta uso wake Mungu Baba atakupa chochote utakacho yeye ni mwaminifu
Bwana anasikia maombi ya wenye haki atajibu Bwana hatawanyima kitu chochote X3