Shilingi Yaua Tena Maua - Simba Wanyika



     
Page format: Left Center Right
Direct link:
BB code:
Embed:

Shilingi Yaua Tena Maua Lyrics


Shilingi Yauwa Tena Mauwa
Ama kweli dunia ooh dunia
Ooh wake kwa waume
Baba ooh twasumbuka
Enzi ya Adamu na Eva
Dunia ilikuwa nzuri
Enzi ya Adamu na Eva
Dunia ilikuwa nzuri iyaah
Lakini dunia ya leo
Bila kuwa na pesa
Hakuna sauti mama
Ooh kusikika iyaah
Iwe mwanamke au iwe mtoto
Iwe mzee kila mtu mawazo yake mikopo
Aah Stella
Sasa ninashangaa ninapoona dunia

Kila mtu yuko mbio kutafuta shilingi
Kila mtu yuko mbio kutafuta shilingi iyaa
Hata ukiona hapo *Mbindo anapohangaika
Mawazo yake yote yako kwa shilingi iyaa
Uwe na sura nzuri baba ya kupendeza
Kama huna shilingi mambo yako ni bure iyaa
Mapenzi ya zamani yalikuwa ni bure
Zamani za kale mambo yalikuwa shwari
Lakini kisirani shilingi baba ikaharibu
Sasa hakuna cha bure dunia baba ni shilingi
Hata mtoto mchanga yule aliyezaliwa leo
Anapolia mama eeh mama eeh mama
Hebu tupa shling pale atakuonyesha pengo
Ama kweli shilingi ni sabuni ya roho
Hata kama una mawazo shilingi itakusafisha roho
Aah jamani
Hata yule mnyama yule wa siku hizi
Hebu tupa shilingi pale pale baba atakurarua
Iwe mzee wa miaka baba hamsini
Bora awe na shilingi warembo watamwandama
Na wewe kijana utaachwa hapo hapo iyaa
Ooh jamani
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi ni tamu baba usiidharau
Hiyo shilingi moja inaweza kuvunja mlima
Hiyo shilingi moja inaweza ulale pakubwa
Usidharau shilingi baba yaua
Mama ooh ooh
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua
Katikati ya mapenzi bila shilingi ni bure
Weye useme yote bila mapesa ni ngumu
Hata uwe na sura ya kupendeza baba ni ngumu
Bora uwe na shilingi mambo yako yatanyooka
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi itakufanya weye baba uimbe
Tena shilingi itakufanya uwe ofisa
Hata ukiwa na miaka ishirini na tano baba
Pale pale utaitwa mzee
Pale pale utaitwa mzee wa shilingi
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua yeeh
Ooh
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua
Hakika shilingi ni kitu baba bora
Hiyo shilingi moja itakufanya baba usipande basi
Usidharau shilingi baba yang’ara
Katikati ya roho binadamu baba yang’ara iyee
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua eeh
Ukitaka chochote dunia baba ni shilingi
Ukiwa na mpenzi wako ooh maneno tupu
Hayavunji mfupi wewe bwaga shilingi mezani
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua
Mambo yafike magumu hayapitiki
Kati ya mapenzi hata useme mazuri
Lakini ukiona mwanamke anapita vile na vile
Weye toa shilingi juu weye utakubaliwa sana
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua
Shilingi yaua ooh tena maua iyaah aah
Lyrics Submitted by Trust Jeferson

Enjoy the lyrics !!!

Simba Wanyika was a Kenyan based band created in 1971 by Tanzanian brothers Wilson Kinyonga and George Kinyonga, and disbanded in 1994. Simba Wanyika and its two offshoots, Les Wanyika and Super Wanyika Stars, became some of the most popular bands in Kenya. Their guitar-driven sound, inspired by the Soukous guitarist Dr. Nico, combined highly melodic rumba with lyrics sung in Swahili. Simba wa nyika means "Lions of the Savannah" in Swahili.

Read more about Simba Wanyika on Last.fm.


User-contributed text is available under the Creative Commons By-SA License and may also be available under the GNU FDL.

View All

Simba Wanyika